Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafunzi wavalishwa maboksi wasipige chabo

Monday , 21st Oct , 2019

Chuo cha The Bhagat Pre-University College, kilichopo nchini India kimeomba msamaha kufuatia kitendo cha kuwavalisha maboksi, Wanafunzi ili kuzuia kupiga chabo wakati wa majaribio ya zoezi hilo.

Taarifa za chuo hicho kufanya tukio hilo, zilisambaa baada ya kupostiwa katika mtandao wa kijamii wa Facebook na mmoja wa wafanyakazi katika chuo hicho ambazo zilionesha wanafunzi wamevaa maboksi, huku sehemu ya mbele la maboksi hayo yapo wazi.

Msamamizi mkuu wa chuo hicho, MB Satish, amesema walitumia njia hiyo kukabiliana na udanganyifu wa kupiga chabo kwa wanafunzi na walifanya hivyo kama jaribio la muda tu kisha waliwatoa maboksi hayo kichwani.

"Hakuna mwanafunzi aliyelazimishwa kuvalia boksi kichwani. Kama unavyoona katika picha hizi kuna baadhi ya wanafunzi ambao hawajazivalia, Waliokuwa wamevalia pia baadhi yao walivua baada ya dakika 15, wengine baada ya dakika 20 na hata sisi wenyewe tuliwambia wazivue baada ya saa moja" amesema MB Satish 

 

"Kati ya wanafunzi 72 ni 56 ndiyo walivaa maboksi kama sehemu ya majaribio, walisema wanajisikia vizuri na jaribio hilo na chuo hakijamsumbua mwanafunzi yeyote kuhusu suala la kuvaa maboksi hayo" ameongeza. 

Mamlaka ya usimamizi wa shule nchini India iliamuru chuo hicho kutoa ufafanuzi wa maelezo na kuomba  msamaha juu jaribio hilo.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine