Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uhamisho wa aina hii kwa walimu wapigwa marufuku

Tuesday , 22nd Oct , 2019

Kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya upungufu wa walimu katika maeneo ya vijijini mkoani Morogoro, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loatha Ole Sanare amepiga marufuku walimu waliopo maeneo ya vijijini kuhamishiwa manispaa ya Morogoro bila kufuata utaratibu.

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Loatha Ole Sanare.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa agizo hilo  kwenye kikao kilichowakutanisha Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa halmashauri pamoja na maafisa taaluma wa halmashauri zote mkoani humo, ambapo amesema kuwa hali hiyo ni moja ya sababu inayochangia baadhi ya shule kufanya vibaya kutokana na upungufu wa walimu.

Ole Sanare ameongeza kuwa, uhamisho usiofuata taratibu umechangia kuwepo kwa upungufu mkubwa wa walimu kwenye shule za msingi na sekondari zilizopo kwenye maeneo hayo.

Aidha Mkuu wa Mkoa Ole Sanare amesema kuwa amepata taarifa ya kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya ofisi za kitendaji mkoani hapa hivyo  amewataka watendaji kushirikiana ili kutatua changamoto zilizopo.

Kwa upande wao baadhi ya watendaji kwenye halmashauri mkoani hapo wamesema kuwa kuna baadhi ya shule zilizopo maeneo ya vijijini zina walimu wachache, hivyo maagizo ya Mkuu wa Mkoa yatasaidia kuboresha sekta ya elimu mkoani Morogoro.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine