Akizungumza mahakamani hapo leo Novemba 7, 2019, Wakili Mwandamizi wa Serikali Wankyo Simon, mbele ya Hakimu Mkazi Vicky Mwaikambo, amesema kuwa kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.
Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu, likiwemo la utakatishaji wa fedha zaidi ya Shilingi milioni 173, uhujumu uchumi na ukwepaji wa kodi.
Kabendera alikamatwa nyumbani kwake Mbweni, Jijini Dar es Salaam, na watu waliodaiwa kuwa ni maafisa wa Polisi, Julai 29, 2019.