Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bashiru Ally adai Maalim Seif anapotoshwa

Wednesday , 4th Dec , 2019

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally, amesema Mshauri Mkuu wa ACT - Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, kuna kauli ambazo amezieleza hazikutokea kwenye ziara yake anayoifanya hivi sasa Visiwani Zanzibar, ambapo alidai kumeandaliwa mpango wa kuhakikisha yeye hagombei

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally.

Urais wa Zanzibar kupitia chama chake kipya.

Bashiru Ally ameyasema hayo wakati akizungumza na wanaCCM Mkoa wa Kusini Pemba, alipokuwa akizindua tawi la Ole, jimbo la Ole, ambapo amesema ziara yake ya siku tisa katika Visiwa vya Unguja na Pemba, ina lengo la kuimarisha uhai wa chama na si vinginevyo.

"Maalim Seif hakuwahi kwenye matamko yake ama mikutano yake kunizungumzia kwa ukali na chuki kiasi kile kama alivyofanya, hivyo kama mitambo tu nimeifunga siku tisa mitetemeko hii imeanza kusababisha taharuki, je ikianza kufanya kazi itakuaje, mimi sitaki kumjibu maana kwa bahati mbaya anawashauri wabaya kwa sababu kwa kasi ya ziara yangu asingewezea kufuatilia bila kuwatuma watu, na ziara yangu kote imekuwa hadharani na vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti, nimeshangaa kusikia mambo ambayo hayakutokea kwenye ziara yangu" amesema Katibu Mkuu CCM.

Aidha Bashiru Ally amesema kuwa "katika hili niwaase wanaCCM na Watanzania msimhukumu Maalim Seif kwa kuwa hata yeye anapotoshwa na wanaomshauri, tangu awe mshauri amekuwa hatafuti tena taarifa za kweli, kila anachopokea anakwenda kuropoka".

Hivi karibuni akizungumza na vyombo vya habari Visiwani Zanzibar, Maalim Seif alidai kuna baadhi ya njama zimepangwa ili kumkosesha yeye uhalali wa kugombea Urais kwenye Uchaguzi wa 2020.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu