Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Aliyeiba nguo za ndani 100 akutwa amevaa 2

Wednesday , 4th Dec , 2019

Mwanaume mmoja mwenye tabia ya Wizi wa nguo za ndani za wanawake, anayejulikana kwa jina la Mukoshi Chipukosia (36), kutoka kijiji cha Hirumbi nchini Kenya, amekamatwa na kufikishwa kwa Mjumbe wa Nyumba Kumi kwa kosa la kuwaibia wanawake nguo za ndani 100 na kukutwa amevaa mbili.

Picha ikionesha Nguo za ndani

Kwa mujibu wa Mjumbe wa Nyumba Kumi amesema, mwizi huyo amekutwa hadharani akiwa amevaa nguo hizo, wakati anajaribu kuiba zingine kwenye kamba na ndipo Mbwa wa ulinzi wa eneo hilo akaanza kubweka na kumshtua mmiliki.

Aidha mmoja wa wamiliki wa nguo hizo amesema, alikuwa anachunga Ng'ombe ghafla akasikia Mbwa wake anabweka na alipoenda akamkuta mwizi huyo anaiba.

"Tumechoshwa na hii tabia, anachofanya sio tabia nzuri, anaiba nguo za ndani za wanawake pekee, kwanini isiwe na za wanaume, kila mara anatuibia sisi tu inatushangaza ni aina gani ya wizi huu bora angeiba Kuku, Mbuzi au Ng'ombe ila sio nguo za ndani imetushtua sana" amesema mmoja wa waathirika wa wizi huo.

Pia mwizi huyo amejitetea kwa kusema yeye ni maskini, hana pesa za kununua nguo za ndani za kiume kwa hiyo ilikuwa inamlazimu kuiba na kuahidi kuwa hatorudia tena.

Chanzo ni Tuko News na K24 Tv.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine