Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kifo cha kiongozi wa Oman kilitabiriwa

Saturday , 11th Jan , 2020

Sultan wa Oman Qaboos bin Said amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Januari 11, 2020. Taarifa ya kifo cha Qaboos imetolewa na TV ya taifa ambapo pia zimetangazwa siku 3 za maombolezo pamoja na siku 40 za bendera kupepea nusu mlingoti. Sultan Qaboos amefariki akiwa na umri wa miaka 79.

Sultan wa Oman Qaboos bin Said

Kupitia EATV & EA Radio Digital, tumekuandalia historia fupi ya maisha ya Sultan Qaboos bin Said na ugonjwa ulioutoa uhai wake.
 
Maisha yake ya awali

Kiongozi Sultan Qaboos bin Said amezaliwa Novemba 18, 1940 na kufariki Januari 10, 2020, amekaa madarakani kwa muda wa  miaka 50, alianza kuiongoza Oman mwaka 1970 hadi umauti unamkuta alikuwa yupo katika uongozi.

Ameweka rekodi ya kukaa madarakani kwa muda mrefu katika nchi za Mashariki ya kati hadi kwenye nchi za falme za kiarabu.

Maisha Binafsi

Sultan Qaboos Bin Said ni mtoto pekee katika uzao wa baba yake ambaye alikuwa kiongozi wa Oman aitwaye Sultan Said bin Taimur na mama yake Sheikha Mazoon al-Mashani, alioa wake watatu katika nyakati tofauti  na katika maisha yake hajawahi kupata mtoto wala ndugu wa kuzaliwa naye tumbo moja.

Elimu

Elimu ya msingi na sekondari alipata katika shule ya Salalah, kisha akahamishiwa shule binafsi ya St Bury St Edmunds nchini Uingereza akiwa na umri wa miaka 16, alivyofikisha miaka 20 alijiunga na chuo cha ufalme wa kijeshi na alipohitimu kozi hiyo mwaka 1962 alijiunga katika jeshi la Uingereza.

Ugonjwa na Kifo

Kuanzia mwaka 2015 alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya Saratani ya utumbo mpana "Colon Cancer", hadi kufikia Disemba 14,2019 kutoka katika hospitali ambayo ilikuwa inampa matibabu UZ Leuven nchini Ubelgiji, ilitangaza kuwa hatachukua muda mrefu wa kuishi duniani, ambapo yeye mwenyewe alitaka arudishwe nyumbani ili umauti ukimfika umkutie akiwa kwao.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu