Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sheikh aoa mwanaume mwenzake agundua baada ya wiki

Tuesday , 14th Jan , 2020

Sheikh mmoja nchini Uganda aliyejulikana kwa jina la Mohamed Mutumba wa Msikiti wa Kyampisi Masjid Noor, uliopo katika wilaya ya Kayunga, amesimamishwa kufanya kazi hiyo baada ya kumuoa mwanaume mwenzake akidhani ni mwanamke.

Sheikh Mohamed Mutumba na mwanamke feki Swabullah Nabukeera.

Wawili hao waliishi kama mume na mke kwa wiki mbili, bila ya Sheikh kutambua jinsia kamili ya mke wake, ambapo baadae ukweli ulijitokeza baada ya polisi kumkamata mwanamke huyo feki kwa madai ya wizi, wakati wakimfanyia ukaguzi na kugundua alikuwa na jinsia ya kiume.

Akifanyiwa mahojiano na polisi mwanamke huyo feki aliyekuwa akijulikana kwa jina la Swabullah Nabukeera, aliwaambia jina lake kamili ni Richard Tumushabe wala sio Swabullah Nabukeera kama ilivyokuwa ikijulikana. 

Kwa upande wake Sheikh Isa Busuulwa, ambaye ni Imam Mkuu wa Msikiti wa Masjid Noor Kyampisi, amesema kuwa baada ya siku Nne alipokea malamiko kutoka kwa bwana harusi dhidi ya mke wake huyo kukataa kuvua nguo, na kwamba alifikia maamuzi ya kumsimamisha kazi Sheikh Mutumba ili kulinda heshima ya Dini ya Kiislamu.

"Siku nne baada ya harusi yao, Bwana harusi alikuja kulalamika kuwa mkewe alikataa kuvua nguo wakati walikuwa wamelala, nilikuwa napanga kuenda kwao kuwafanyia ushauri kisha nikasikia tena bibi harusi alikuwa amekamatwa kwa wizi wa runinga na nguo za jirani yao" amesema Sheikh Busuulwa.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine