Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanandoa wauawa kwa kucharangwa mapanga

Friday , 17th Jan , 2020

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera linawashikilia watu saba ambao ni Sophia Joseph, Joseph Magambo, Alphonce Karoli, Martine Makabe, Alex Leopord, Salvatory Mwiliza na Aloyce Leopord kwa tuhuma za mauaji ya wanandoa wawili huku chanzo kikielezwa kuwa ni mgogoro wa ardhi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Revocatus Malimi.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Revocatus Malimi, amesema kuwa tukio hilo lilitokea Januari 14, 2020, majira ya saa 7:00 usiku, katika Kijiji cha Mabale, Kata ya Nyakahura wilayani Biharamulo, ambapo wanandoa hao walikuwa wamelala na ndipo walipovamiwa na kundi kubwa la watu na kuanza kuwacharanga mapanga sehemu zao mbalimbali za miili yao.

"Kabla ya tukio hilo, kulikuwa na mgogoro wa ardhi kati ya marehemu na baadhi ya wana ukoo kwa muda mrefu, uliotokana na kuachiwa eneo alilokuwa akiishi na Babu yake, aliyehama kwa shinikizo la wana jamii waliomtuhumu kuwa ni mwizi" amesema Kamanda Malimi.

Wanandoa hao waliopoteza maisha yao ni Elizeus Rubanie (35) na mke wake, Juliana Joseph (28), na kwamba upelelezi utakapokamilika watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani.
 

HABARI ZAIDI

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12