Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

JPM aeleza ndoa ya mteule wake ilivyotaka kuvunjwa

Monday , 3rd Feb , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, ameeleza ni kwa namna gani ndoa ya aliyekuwa Kamishna wa Ardhi Mary Makondo, ilivyotaka kuingia mashakani kutokana na watu wengi kumchukia, sababu ya misimamo yake aliyokuwa nayo.

Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, kulia ni Mary Makondo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi.

Rais Magufuli ameyabinisha hayo leo Februari 3, 2020, wakati akieleza ni kwa namna gani anawafahamu viongozi walioapishwa leo Ikulu ya Jijini Dar Es Salaam, ambapo Mary Makondo, yeye ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kusema kuwa ataenda kuinyosha vizuri wizara hiyo kwa kuwa ina madudu mengi.

"Hawakumpenda sana kwa sababu ya misimamo yake na kwasababu hiyo nikasema huyu ambaye hawampendi ndiye atabaki palepale ili wale ambao hawampendi waumie vizuri sana, wamejitahidi pia kumuandikia vimeseji vya kumchafua na walitaka kumchonganisha na mume wake, nampongeza mume wake aliendelea kusimama imara" amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amewapongeza wale wote walioapishwa na kuwataka wakafanye kazi kwa weledi huku wakisimamia maslahi ya nchi na Taifa kwa ujumla.
 

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu