Winga Benard Morrison akisaini mkataba wa kuitumikia Klabu ya Simba
Uongozi unafuatilia kwa karibu na umakini mkubwa suala hilo na ikithibitika hatua kali na za mfano zitachukuliwa kwa pande zote zinazohusika.
Aidha Uongozi unawataka wanachama na wapenzi wa Yanga kuwa watulivu kwani mchezaji Benard Morrison ana mkataba na Klabu hiyo hadi 2022 na shauri baina yake na Klabu bado liko mikononi mwa Shirikisho la Soka Tanzania na Jumatatu linaendelea kusikilizwa.