Friday , 14th Aug , 2020

Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji ya shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) kupitia kwa Mwenyekiti wake Elias Mwanjala imewasilishwa malalamiko kwa kamati ya maadili dhidi ya wanafamilia watatu.

Mjumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF, Zacharia Hans Poppe akiwa katika moja ya mechi ya Klabu yake ya Simba.

Afisa habari wa Klabu ya Simba Haji Manara, Mjumbe wa kamati hiyo Zacharia Hanspope na Mchezaji Benard Morisson kwa kuchochea hisia kwa Jamii na kutoa vitisho kuhusu shauri la Klabu ya Yanga na Benard Morisson.

Pia sekretarieti ya TFF imempeleka Afisa habari wa Klabu ya Yanga Hassan Bumbuli Katika kamati ya maadili ya TFF kwa kutoa Taarifa uongo. Wahusika wote watapewa malalamiko yao kwa maaandishi na wito wa kuhudhuria kikao cha kamati ya maadili.