Sunday , 11th Oct , 2020

Katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike duniani Mgombea mwenza kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu, amesema kuwa mtoto wa kike ana haki ya kusikilizwa na kupewa nafasi kama mtoto wa kiume.

Mgombea mwenza kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu

Samia Suluhu amesema hayo leo Oktoba, 11, katika viwanja vya Muze Sumbawanga, Mkoani Rukwa, katika muendelezo wa kampeni zake nakuongeza kuwa  watoto wa kike wakisikilizwa inawajengea mazingira bora ya baadae.

"Kimataifa leo ni siku ya mtoto wa kike,tunachokisema hapa mtoto wa kike anahaki ya kupewa nafasi,kupata matibabu,kusikilizwa matakwa ya moyo wake kama mtoto wa kiume’’Samia Suluhu

Pia mgombea mwenza huyo ameendelea kunadi sera za chama chake  ambapo ameahidi kushughulikia changamoto ya barabara na pindi  ujenzi  utakapokamilika utasaidia kuimarisha uchumi pamoja na kusaidia sekta ya usafiri na usafirishaji

"Napenda niwape taarifa ya faraja tunakwenda kuongeza uwezo wa TARURA  kitaalamu lakini pia kifedha ili waweze kushughulikia barabara zinazowahusu tunajua ni taasisi tumepanga kwenda kuiimarisha’’Samia Suluhu  

 Aidha katika kuadhimisha siku hii East Africa Tv, na East Africa Radio, wamefanya matembezi ya hisani katika wilaya ya Kisarawe wakiungana na wadau mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo, lengo ikiwa ni kumbakiza mtoto wa kike shuleni  kwa kumpatia taulo za kike.