
Pichani tuta la udongo lililowekwa na wananchi kuzuia ajali.
Wakiongea leo na Kurasa wananchi hao wamesema kwa siku wanagongwa watu wasiopungua watatu na wengine wanapoteza maisha.
Kwa upande wake mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Yombo Rahim Maridadi, amesema ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko ya wananchi hao mara kwa mara na kuyafikisha kwa wahusika lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.