Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli aeleza alivyomjengea barabara Msuya

Wednesday , 21st Oct , 2020

Katika muendelezo wa kampeni za urais Tanzania, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi Dkt John Magufuli ameeleza sababu zilizofanya asimamie kikamilifu ujenzi wa Barabara ya kwenda kwa Waziri Mstaafu Cleopa Msuya wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi Dkt John Magufuli

Magufuli ameyaeleza hayo leo kwenye mkutano wa kampeni wilayani Mwanga, ambapo amesisitiza kuwa watu walimshangaa lakini ukweli kuwa anapoishi Msuya pia kuna watu wanaishi na barabara hiyo wanatumia wote hivyo ni maendeleo kwa wote.

''Nashukuru sana kwa mapokezi hapa Mwanga, huwezi kuitaja historia ya Mwanga bila kumtaja mzee Cleo[a Msuya, nikiwa waziri wa Ujenzi nilisimamia ujenzi wa barabara ya kwenda kwake, watu walihoji sana lakini historia yake kwenye taifa hili haiwezi kufutika'' - amesema Magufuli.

Aidha amemuonya mkandarasi anayejenga mradi wa maji katika wilaya za Mwanga na Same kwa kumtaka akamilishe haraka vinginevyo atamfukuza.

''Nimekuwa waziri wa Ujenzi najua makandarasi wanasimamiwaje, huu mradi wa maji hapa Mwanga naomba niwaambie sasa nitausimamia mwenyewe na nimemwambia mkandarasi ndani ya mwezi mmoja aniambie anaukamilishaje, asipofanya hivyo namfukuza hamtawaona tena'' ameongeza.

Pia ameahidi kuwajengea hospitali ya wilaya. ''Hapa Mwanga najua mna jambo lenu la ubaguzi mara hawa Wasangi na wale Wagweno lakini mimi najua sisi wote ni watanzania na kwasababu mnahitaji Hospitali nitawajengea Hospitali ya Wilaya hapa Mwanga na sio mbaya Usangi kuwa na hospitali ya wilaya na Mwanga mkawa nayo'', amesema Magufuli.
 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine