
Aliyekuwa Kocha msaidizi wa Simba, Denis Kitambi enzi zake akiwa anafundisha kikosi cha mabingwa watetezi wa VPL.
Kauli hiyo imetolewa na aliyekuwa kocha msaidizi wa klabu hiyo, Denis Kitambi ambaye alikuwepo kwenye benchi la ufundi la Simba ambayo ilicheza robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika misimu miwili iliyopita.
''Kwakweli licha ya kupata matokeo mchanganyiko msimu huu lakini hakuna kikosi kinachoifikia Simba kwa ubora hapa Tanzania, wamekaa na wachezaji kwa muda mrefu na wanacheza mpira wa kuvutia hivyo bado wana nafasi ya kufanya lolote msimu huu'' alisema Kitambi.
Kitambi ambaye aliwahi kuifundisha Azam kama kocha msaidizi wa Stewart Hall, alifanya kazi nchini Kenya kabla ta kurejea nchini Tanzania kuifundisha Simba.
Simba kwa sasa inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ikiwa na alama 16 baada ya mechi 8 huku ikiwa imefungwa michezo miwili na sare mmoja.