
Makusu Mundele akiwa katika mkutano na waandishi wa habari
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28, alikuwa akihusishwa na klabu ya Yanga ya Tanzania, amesema amefurahi kujiunga na miamba hiyo ya Afrika ambayo inahistoria nzuri katika michuano ya vilabu.
Mundele ambaye aliwahi kucheza soka la kulipwa nchini Ubelgiji, Misri, Algeria na Hungary, anategemewa kuisaidia Pirates katika michuano ya kombe la shirikisho Afrika msimu huu.