Monday , 23rd Nov , 2020

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard Akwilapo amewataka watumishi wanaokaribia kustaafu kutunza kumbukumbu zao ilikuepuka kupata shida yakulipwa mafao yao huku akiahidi kuhakikisha michango ya watumishi  waliopo chini ya wizara hiyo inawasilishwa kwa wakati.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard Akwilapo

Hayo yamesemwa leo  katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Morogoro  mjini wakati akifungua  mafunzo maalumu ya watumishi  wanaotarajia kustaafu  wapatao 223  kutoka makao makuu ya wizara , Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ,Vyuo vya Ualimu  na Idara ya udhibiti wa shule  ambao wapo  chini ya wizara hiyo ambao ameahidi serikali itahakikisha michango ya watumishi  waliopo chini ya wizara hiyo inawasilishwa kwa wakati kwenye Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).  

“Kwa sasa hivi tunahakikisha tunapitia kumbukumbu za kila mtumishi  ili kuona  mchango wa  kila mwezi inaenda ,huko nyuma kulikuwa na tatizo kidogo  palikuwepo na madeni ya ajabu ajabu , lakini  hivi sasa mambo  yamenyooka   ni kutokana na mfumo uliowekwa “ alisema Dk. Akwilapo.

Aidha Dk Leonard Akwilapo amesema kuwa kwa kutunza kumbumkumbu kutasaidia watumishi wanapofikia umri wa kustaafu wapate mafao  yanayostahiki  kwa wakati ambayo yatawawezesha kushiriki  shughuli za maendeleo ya kupitia miradi ya kiuchumi watakayoianzisha .

Dk. Akwilapo, aliwaagiza watendaji wa wizara hiyo kuhakikisha wanapitia nyaraka zote za watumishi ili kuona   mapungufu yanayojitokeza  na kama kuna changamoto na ziweze kurekebishwa kabla ya kufikia Juni mwaka 2021  kwa lengo la kuzirekebisha  kasoro hizo.