Wednesday , 2nd Dec , 2020

Ni updates za msanii wa BongoFleva Wini Tz ambaye amesema licha ya wasanii wa kike kutongozwa na ma-producer au 'directors'  pia wana gharama sana kwenye muziki kuliko wasanii wa kiume.

Msanii wa BongoFleva Wini Tz

Wini Tz amesema msanii wa kike anatakiwa apendeze kila wakati asipokuwa na menejmenti au sapoti itampa ugumu kushine ambapo akajitolea mfano kwa kusema aliwahi kununua nywele za gharama ya Milioni 1.

"Kwangu mimi kutongozwa sio changamoto kubwa kwa sababu sijaanza kutongozwa kwenye muziki ila najua jinsi ya kukabiliana na hiyo ishu, kwenye muziki kuna changamoto nyingi kuliko za kutongozwa kwanza wasanii wa kike tuna gharama kuliko wasanii wa kiume,  kama anakuwa hana menejmenti au sapoti inakuwa ngumu kwake" amesema Wini Tz

Aidha msanii huyo ameendelea kusema "Vitu ni vingi kwa msanii wa kike anatakiwa apendeze kila wakati ila mimi napendaga kuwa 'natural', kitu cha gharama ambacho niliwahi kununua ni nywele zangu za milioni 1 na laki 2

Zaidi tazama hapa chini kwenye video