
Msanii Barnaba Classic
Akijibu kuhusiana na hilo Barnaba Classic amesema yule ni baba yake mzazi ila anachokiamini hana tatizo lolote na baba yake japo alikuwa hajui kinachoendelea.
"Yule ni baba yangu mzazi kabisa wala sio jambo la kiki , waswahili wanasema mzazi hakosei, hasemwi na hakosolewi, ukiachana na hayo mnayoyasikia mimi sina tofauti wala matatizo na baba yangu, namshukuru Mungu kwa kila jambo ila sitaki kulizungumzia sana suala hili nilikuwa sijui kinachoendelea" amesema Barnaba Classic
Ziaidi tazama hapa chini kwenye video.