Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Dar es Salaam kuna mapungufu, RC yupo"- Magufuli

Monday , 18th Jan , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli, amesema kuwa atakaporudi Dar es Salaam, akute ujenzi wa shule ya msingi Barango, iliyopo wilayani Ubungo iwe imekamilika na wanafunzi wawe wanakaa kwenye madawati.

Kushoto ni Rais Dkt. John Magufuli na kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaa, Aboubakar Kunenge

Agizo hilo amelitoa hii leo Januari 18, 2021, mjini Bukoba, mkoani Kagera mara baada ya kufungua shule ya wavulana ya Ihungo iliyopo mkoani humo , ambapo ameshangaa kuona viongozi ndani ya mkoa huo wapo akiwemo Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge na kuongeza kuwa hali hiyo inaonesha kuwa alikosea kuchagua viongozi.

"Hata Dar es Salaam kuna mapungufu kuna shule moja ya msingi Ubungo inaitwa Barango, ina wanafunzi wengi tu na bado wanakaa chini madarasa mengine yamebomoka, madawati yamevunjika na yameachwa bure, Mkuu wa wilaya yupo, Mkuu wa mkoa yupo, Mkurugenzi na mbunge wa Ubungo yupo na ni Profesa wa Elimu lakini hiyo shule wanafunzi wanakaa chini", amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa, "Ninamshukuru mwandishi ameitoa kwenye mitandao na viongozi wa kule wakaanza kusema ni masuala ya kisiasa hayo si masuala ya kisiasa hayo ndiyo mimi ninapenda kuyajua, ninazungumza nikiwa Kagera lakini nikienda Dar es Salaam nikute madarasa yamekamilika na wanafunzi hawakai chini, nitaenda kuitembelea kama wananisikia wa Dar es Salaam, Message sent and Delivered".

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu