
Wachezaji wa MTC wakishangilia ushindi
MTC ilitoa kichapo cha seti 3-0 dhidi ya Societe Omnisport de Armie na kujiahakikishi kumaliza katika nafasi ya 9-12 miongoni mwa timu 16 zilizoshiriki, hii inatokana na kushindwa kuingia katika robo fainali ya kwanza inayotoa bingwa kutoka makundi manne ya awali
Muundo wa mashindano kuna jumla ya timu 16 zilizokuwa katika makundi 4 vinara wa makundi na wale walioshika nafasi za 2 katika kila kundi wanakwenda kwenye robo fainali ya kwanza (1-8) inayotoa bigwa, robo fainali ya pili inahusisha timu ya (9-16) isiyotoa bingwa ila itasaidia kupanga nafasi ya kila timu toka 1-16
Michuano hiyo mikongwe ya mpira wa wavu Africa, inayofanyika Tunisia ilianza tarehe 18/04/2021 na inatazamiwa kumalizia tarehe 28/04/2021 kwa kumpata bingwa wake