
Rais wa kamati ya maandalizi ya Olympic Tokyo 2020 Seiko Hashimoto
Rais wa kamati ya maandalizi bwana Seiko Hashimoto amesema ''tunatarajia kukutana kabla mwezi huu haujaisha kujadili kiwango cha mashabiki watakao ruhusiwa kuingia viwanjani lakini kwa haraka nachoweza kusema kutakuwa na mashabiki''
''Tutakaa na wenzetu wa Serikali,pamoja na watu wa kamati ya International Olympic Commitee 'IOC'mamlaka mbalimbali kutafuta suluhu ya jambo hili mwisho wa siku tunaamini tutapata muafaka''aliongeza
Mashindano haya ya mwaka huu yanatarajiwa kuanza tarehe 23/07/2021 na kumalizika 8/08/2021 pamoja na kutumia logo ya Tokyo 2020 kufuatia kuhairishwa kwa mashindano haya mwaka jana kutokana na janga la Corona.
Mashindano haya makongwe , yenye umri wa miaka 125 yanatazamiwa kuhusisha michezo tofauti tofauti 339 huku mchezo kivutio sana ikiwa ni riadha