Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nafanya biashara zinazorudisha kwa jamii- Flaviana

Wednesday , 23rd Jun , 2021

Mwanamitindo na Muanzilishi wa Taasisi ya Flaviana Matata FMF, Flaviana Matata amesema hana mpango wakufanya biashara ambayo haigusi wala kurudisha jamii kwani hata katika biashara zake za sasa zinarudisha kwa jamii.

Mwanamitindo na Muanzilishi wa Taasisi ya Flaviana Matata FMF, Flaviana Matata

Mwanamitindo huyo wa Kimataifa amesema hayo leo katika mahojiano yake na kipindi cha Supa Breakfast ambapo amesema anashirikiana na kampeni ya Namthamini ya East Africa Television na East Africa Radio kwa sababu taasisi ya FMF imejikita katika shughuli za kumsaidia na kumuwezesha binti wa kike.

 

“Nilisema sitaki nifanye biashara ambayo haigusi jamii kwa namna yoyote, sisi tunafundisha wasichana namna ya kutengeneza kucha, kwenye taulo za kike 10% inayopatikana tunarudisha kwa jamii, hata biashara tutazoanzisha lazima ziwe zinarudisha kwa jamii,” amesema Flaviana.

Akielezea safari yake mpaka kufika kwenye uwanamitindo Flaviana amekiri kuwa hakutaka kushiriki katika shindano la Miss Universe bali watu wachache walimsukuma akiwemo marehemu Ruge Mutahaba huu akiweka wazi kuwa hana mpango wa kuigiza.

“Miss Universe sikutaka kufanya nilikuwa tomboy, sijui kutembelea viatu ila Marehemu Ruge alinisukuma na dada Irene akanifundisha kuvitembelea, nilivoshinda Miss Universe watu walishangaa kwa sababu walijua nipo kujifurahisha,” amesema Flaviana.

Aidha, Flaviana amesema bado ipo changamoto ya mfumo dume hususan pale viongozi wanavyochaguliwa huku akigusia kelele zilizokuwepo pindi Mhe. Jokate Mwegelo alivyoteuliwa kuwa kiongozi.

“Mfumo dume bado upo, changamoto bado zipo unaona viongozi wa aina fulani wakichaguliwa watu wanaongea, nakumbuka Jokate alivyochaguliwa kulikuwa na kelele nyingi, hata kama alikosea huko nyuma nani hajawahi kukosea kwenye maisha yake ?,” alihoji Flaviana.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali