Heung-Min Son akishangilia moja ya bao aliloifungia Tottenham Hotspurs
Mkataba wa mshambuliaji huyo wa Korea sasa utaendelea hadi majira ya joto mwaka 2025, ambayo itamfanya awe amedumu klabuni hapo kwa miaka 10 baada ya kujiunga na klabu hiyo akitokea Bayer Leverkusen mwaka 2015.
Son mwenye umri wa miaka 29, amefunga magoli 107 na kutoa assist 64 katika mechi 280 alizocheza katika mashindano yote kwa kipindi cha misimu sita aliyoitumikia Tottenham hadi sasa.
Pia son ndio mchezaji aliyefunga goli la kwanza la Ligi Kuu na lile la Ligi ya Mabingwa kwenye uwanja mpya wa Tottenham Hotspur wanaoutumia hivi sasa.