
Mcheza tennisi wa sita kwa ubora duniani kwa wanaume, Dominic Thiem.
Thiem ambaye anashikilia nafasi ya sita kwenye viwango vya ubora vya tenisi duniani kwa wanaume, amesema uamuzi wa kukosekana kwenye michuano hiyo umekuja baada ya ushauri aliopewa na jopo la madaktari wake na kuthibitisha nyota huyo atakuwa nje kwa mwaka mzima.
Mara ya mwisho Thiem kujitupa dimbani ilikuwa ni mwezi Juni mwaka huu kwenye michezo ya Mallorca Open nchini Hispania ambapo alipata maumivu hayo ya mkono.