Monday , 6th Sep , 2021

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi, ameitisha mazungumzo baina ya vyama vya Siasa, Polisi na Ofisi ya Msajili ili kutafuta suluhu ya mivutano ya mikutano ya ndani na makongamano ya kisiasa.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi

Jaji Mutungi ameeleza hayo leo Jijini Dar es Salaam na kusema ameitisha mkutano huo ili kufanya mazungumzo na wadau hao muhimu ili kuondoa sintofahamu iliyoibuka baada ya kudaiwa polisi kuingilia na kuzuia mikutano ya kisiasa ya ndani.

Hatua hiyo imekuja baada ya siku za hivi karibuni Chama cha NCCR- Mageuzi kilinukuliwa kikilalamikia kuzuiwa na Jeshi la Polisi kufanya mkutano wa Kamati Kuu katika eneo la Msimbazi baada ya Polisi hao kuvamia mkutano huo