Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yarejea Dar, kuivaa Simba Septemba 25

Monday , 20th Sep , 2021

Kikosi cha mabingwa wa kihistoria wa Tanzania bara Yanga SC kimerejea nchini leo Asubuhi kikitokea nchini Nigeria ambako kilicheza mchezo wa klabu bingwa Afrika hatua ya awali dhidi ya Rivers United mchezo ambao Yanga ilifungwa 1-0 na kutupwa nje ya mashindano.

Wachezaji wa Yanga wakiwa uwanja wa Ndege

Kipigo hicho kimeifanya Yanga itupwe nje ya mashindano ya klabu bingwa kwa kipigo cha jumla cha mabao 2-0, kwenye michezo miwili wa ugenini na nyumbani, timu hiyo ya wananchi imepoteza michezo yote miwili kwa kufungwa bao 1-0. Kikosi cha Yanga kimerejea na msafara wa watu wote 60 ambao umejumuhisha wachezaji, viongozi na baadhi ya mashabiki.

 

Na kwa mujibu wa ripoti kutoka ndani ya Yanga zinadai kuwa timu hiyo ya wananchi ilikumbana na vitendo visivyo vya kiungwana yani figisu kutoka kwa wenyeji wao, ikiwemo kucheleweshewa majibu ya vipimo vya Uviko 19 na baadae wachezaji wao wanne kutajwa kuwa na Uviko 19 ambao ni Fei Toto, Mukoko Tonombe, Djdgui Diarra na Yacuba Sogne ingawa wachezaji wote hawa walicheza lakini pia Yanga hawakutumia vyumba rasmi vya kubadilishia nguo na badala yake walitumia sehemu ya benchi la kukaa makocha na wachezaji wa akiba uwanjani kama seheumu ya kubadilishia nguo.

Mara baada ya kutupwa nje ya michuano hiyo kikosi cha Yanga kinajikita zaidi kwenye michezo ya Ligi Kuu Tanzania bara na kombe la Azam Sports Federation Cup  na mchezo wao wa mashindano unaofata ni dhidi ya watani zao Simba SC mchezo wa ngao ya Jamii utakao chezwa Septemba 25 katika Dimba la Benjamini Mkapa Da es salaam.

HABARI ZAIDI

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania