Thursday , 7th Oct , 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Mhandisi Aron Joseph, amemkabidhi pesa taslimu shilingi laki tano (500,000) Halfan Athumani, ambaye ni fundi bomba kutoka DUWASA kama zawadi aliyoahidiwa na Waziri wa Maji Jumaa Aweso, kwa kujituma kwake katika kazi.

Kushoto ni Halfan Athumani wakati akizimba bomba, na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA Mhandisi Aron Joseph, akimkabidhi zawadi

Halfan Athuman alionekana katika mtandao wa kijamii wa Instagram kwenye ukurasa rasmi wa Mamlaka ya Majisafi na Mazingira Mjini Dodoma (DUWASA) akifanya kazi ya kuziba bomba kubwa la inchi 16 liliokuwa limepasuka eneo la Chinangali Park jijini Dodoma.

Kwa upande wake Waziri Aweso alipokutana na Halfan kwa mara ya kwanza alimuagiza Mkurugenzi wa DUWASA kumtambulisha kwa bodi ya mamlaka hiyo ili awe katika mipango ya kupewa fursa zaidi katika ngazi yake ya kazi.