Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbadala wa Clatous Chama apatikana Simba SC

Thursday , 14th Oct , 2021

Kocha Msaidizi wa kikosi cha Simba, Mrwanda Hitimana Thierry amesema mchezaji mbadala wa kutengeneza nafasi za mabao klabuni hapo tayari ameshapatikana baada ya Chama kuondoka na wana matarajio makubwa kuwa atafanya vizuri.

Kocha Msaidizi wa Simba, Hitimana Thierry akiwa anasimami mazoezi.

Hitimana ameyasema hayo wakati akizungumzia maandalizi ya mchezo wa kuwania kufuzu hatua ya makundi michuano ya klabu bingwa Afrika ambapo Simba itacheza Jmapili 17, 2021 dhidi ya Jwaneng Galaxy nchini Botswana.

Hitimana amesema, “Katika hizi mechi ambazo tumecheza tumeona jinsi gani tulikuwa tukitengeneza nafasi na kushindwa kuzitumia, lakini mtu wa kutengeneza nafasi ya mwisho, tayari yupo mtu ambaye amepewa jukumu hilo na kuna matarajio makubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo wetu huu"

Maelezo ya Hitimana hayakutaja kwa jina mchezaji huyo mwenye majukumu hayo mapya lakini ripoti za kikachero zinaripoti kuwa ni miongoni mwa kiungo fundi, Larry Bwalya, winga Bernanrd Morrison na Pape Ousmane Sakho. Ikumbukwe kuwa Chama alikuwa kinara wa kutengeneza nafasi za mabao 'Assits' wa Ligi kuu msimu ulioisha 2020-21 kwa kutengeneza nafasi 15 na hata msimu juzi 2019-20 alitoa assist 8 na kuwa kinara katika VPL.

Msimu uliopita Bwalya alikuwa na assist 5 na Bernard Morrison alikuwa na assist 4 licha ya kukosa utulivu na kuwa na ingia toka kwenye kikosi cha kwanza ilhali Sakho alikuwa mchezaji bora wa Lgi kuu ya Senegel.

Kwa upande mwingine amegusia mazingira ya nchini Botswana ambayo wanajiandaa kukabiliana nayo.

“Tumejiandaa vizuri kimbinu na kiufundi, pia tumeshajua tutaenda kucheza kwenye joto kali, tumeanza kulifanyia kazi hilo na kuzoea hali hiyo kabla ya kuondoka kuelekea Botswana". Amesema Hitimana.

Simba inataraji kuondoka nchini Tanzania Ijumaa ya 18, 2021 kuelekea nchini Botswana kwa ajili ya mchezo huo.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90