Tuesday , 19th Oct , 2021

Kampuni ya Uber na Boeing ambao wamejikita katika utengenezaji wa magari yanayopaa maarufu kama eVTOL (electric vertical take-off and landing), wamepanga mpaka kufika mwaka 2040 wawe wameingiza sokoni magari 430,000 ya aina hiyo yatakayokuwa yakitoa hudumu kote duniani.

Picha ya Teksi inayopaa ya umeme inaonekana kama helikopta ikiwa na mabawa ya ndege

Tayari mpaka sasa kampuni ya Joby Aviation ya huko California, ambayo iko mstari wa mbele kuunda teksi zinazopaa imefanikiwa kufanya majaribio 1,000 kwa magari ya eVTOL.

Magari yanaweza kupaa kwa kuinuka na kutua kwa kushuka, na hivyo uwanja unaohitajika utakuwa wa aina mpya.