Wednesday , 27th Oct , 2021

Siku tatu baada ya baa maarufu ya The Cask iliyopo ndani ya jengo la kibiashara la Rock City Mall kuteketea kwa moto, Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Mwanza limebaini chanzo cha kuzuka kwa moto huo kuwa ni hujuma iliyofanywa na watu wasiojulikana bila kuwepo kwa sababu yoyote.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto mkoani Mwanza,Ambwene Mwakibete

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto mkoani Mwanza Ambwene Mwakibete, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini humo, na kusema jeshi hilo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi bado wanaendelea na uchunguzi zaidi ili kuweza kuwabaini waliofanya njama hizo za kuteketeza baa hiyo

Aidha Mwakibete amekanusha kuwepo kwa taarifa za upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii zinazosema gari la zimamoto lilifika katika eneo la tukio bila  kuwa na maji.