Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo Oktoba 28, 2021, jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kitabu kinachoitwa Tanzania Gender Bench Book on Women’s Rights, kilichoandaliwa na chama cha wanasheria na majaji wanawake nchini Tanzania (TAWJA).
"Hata sehemu za kazi unaweza kumuona mwanamke mwenzio kaingia kazini asubuhi uso haukunjuki vizuri ukimuambia moja anakujibu tatu ukimuita chemba ukimuuliza tatizo limetoka nyumbani, kwahiyo unyanyaswaji unafanya wanawake wasi-perform vizuri", amesema Rais Samia
Aidha Rais Samia akasisitiza, "Afadhali wanaume akikereka huko ana njia zingine za kupita akafurahi na akarudi kazini ametulia, lakini sisi hatuna, ni nyumbani kazini, kazini nyumbani, so handle with care sisi ni assets muhimu".






