Sunday , 13th Feb , 2022

Kamati ya kuchunguza tukio la moto ulioteketeza Soko la Mbagala Rangi Tatu usiku wa kuamkia leo Februari 13, 2022 imepewa siku tatu hadi nne. 

Baadhi ya maeneo ya soko hilo wakati moto ukiwaka

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Jokate Mwegelo, ameeleza ambao ameongeza kuwa wafanyabiashara watarudi sokoni kufanya biashara uchunguzi ukikamilika.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeendelea kuhakikisha linadhibiti moto huo usilete madhara zaidi katika maeneo ya jirani na soko kwa kuzima mabaki yote ya moto huo.