Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 20, 2022, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere akitokea nchini Ubelgiji.
"Tukiwa Ufaransa kuna vijipesa tumevipata kwa ajili ya kumalizia njia za mwendokasi na kilimo, waliniuliza kwani haiwezekani Dar au Dodoma kukawa na mabasi mbali na hayo ya mwendokasi kukawa na yanayoenda kwa umeme?, nikawaambia inawezekana kwahiyo hilo lipo kwenye mazungumzo baadaye na sisi tutakuwa kama Ulaya, nadhani miaka mitano, au sita ijayo tunaweza kufika huko," amesema Rais Samia






