Sunday , 20th Feb , 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kwamba huenda ndani ya kipindi cha miaka mitano ama sita ijayo Tanzania itakuwa kama Ulaya, kwani upo mpango wa kuwepo kwa mabasi yanayotumia umeme kati ya mkoa wa Dar es Salaam ama Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Kauli hiyo ameitoa hii leo Februari 20, 2022, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere akitokea nchini Ubelgiji.

"Tukiwa Ufaransa kuna vijipesa tumevipata kwa ajili ya kumalizia njia za mwendokasi na kilimo, waliniuliza kwani haiwezekani Dar au Dodoma kukawa na mabasi mbali na hayo ya mwendokasi kukawa na yanayoenda kwa umeme?, nikawaambia inawezekana kwahiyo hilo lipo kwenye mazungumzo baadaye na sisi tutakuwa kama Ulaya, nadhani miaka mitano, au sita ijayo tunaweza kufika huko," amesema Rais Samia