Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy
Jeshi la Urusi limeshambulia miundombinu ya kijeshi ya Ukraine pamoja na kujeruhi baadhi ya wanajeshi waliopo mpakani, huku matumaini makubwa pia wakiyapata baada ya Rais wa Marekani Joe Biden, kuahidi kushirikiana na Ukraine katika vuguvugu hilo dhidi ya Urusi.
"Kuanzia leo naomba mtulie majumbani, jeshi lipo kazini pamoja na vyombo vyote vya ulinzi," amesema Rais Zelenskyy.
Aidha, kwa hali inayoendelea nchini Ukraine hivi sasa watu wengi wanaukimbia mji mkuu wa Kyiv na wengine wanakimbia katika vituo vya treni chini ya ardhi ili kupata makazi.



