
Lucia Minde, Mkurugenzi wa Sheria na Udhibiti kutoka Serengeti Breweries Limited
Minde ametoa kauli hiyo leo Machi 18, 2022, wakati akizungumza kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio na kusema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha wanaongeza asilimia kadhaa ya wanawake kwenye kampuni.
"Tuna kiwanda tulichoanzisha Julai mwaka jana, ambacho kinatengeneza pombe kali Moshi na wafanyakazi wote kwenye hicho kiwanda ni wanawake, yaani kuanzia pale getini walinzi ni wanawake," amesema Lucia.