Friday , 3rd Jun , 2022

Tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC imepitisha jina la George Wajackoyah kuwania Urais wa nchi hiyo baada ya kumzuiwa siku kadhaa zilizopita kutokana na kutokidhi vigezo

Mgombea wa nafasi ya Urais nchini Kenya kea tiketi ya Chama cha Roots George Wajackoyah

Mwanasiasa huyo kutoka chama cha Roots amekuwa maarifu nchini humo kutokana na sera yake ya kutaka matumizi ya bangi yahalalishwe

Mapema wiki hii, usajili wake wa kugombea urais ulikataliwa na tume ya uchaguzi IEBC kwa kukosa sahihi za kutosha, ambapo alihitajika kuwa na sahihi elfu mbili ambapo amewasilisha tena sahihi hizo na kuruhusiwa kugombea