Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Onyango asaini miwili Simba

Thursday , 23rd Jun , 2022

Beki wa kimataifa wa Kenya, Joash Onyango ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kusalia katika klabu hiyo ya Simba SC baada mkataba wake wa awali kumalizika mwisho wa msimu huu.

Beki wa kimataifa wa Kenya, Joash Onyango .

Akizungumza na EATV Onyango amesema kuwa amesaini mkabata wa miaka mwili ambapo ataendelea kuwatumia Simba hadi mwaka 2024.

''Wanasimba watulie kwakuwa sasa tumepoteza ubingwa lakini msimu ujao tumejipanga kufanya vyema katika michuano yote ambayo tutashiriki na kurudisha heshima ilikuwa nayo Simba'' amesema Onyango.

Tangu alipojiunga na Simba, Onyango amecheza sehemu muhimu ya timu akiwa kama beki wa kati ambapo amekuwa akisaidiana na beki kisiki kutoka Congo, Eneck Inonga, Kennedy Juma pamoja na Pascal Wawa ambaye kwasasa hatokuwepo kwenye kikosi cha Wanamsimbazi msimu ujao.

Hata hivyo kulikuwa na hofu juu ya mustakabali wa Onyango baada ya kukosa mechi mbili za mwisho za Simba dhidi ya Mbeya City na KMC huku Mei mwaka jana, vigogo wa Afrika Kusini, Orlando Pirates, walionyesha nia ya kutaka kuwasajili wachezaji hao na aliyekuwa Msemaji wa Simba wakati huo, Haji Manara (sasa Yanga SC) akadai kitita cha Sh100 milioni.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 anakuwa mchezaji wa pili ndani ya klabu ya Simba kuongezewa mkataba ambao wa kwanza ni Aishi Manula ambaye aliongezewa mkataba siku chache zilizopita huku Rally Bwalya, Bernard Morrison na Pascal Wawa wakiondoka klabu hapo.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine