Msemaji wa Idara ya Uhamiaji, Paul Msele
Akizungumza na EATV Msemaji wa Idara hiyo Paul Msele, amesema vitendo hivyo havikubaliki na amewaonya wananchi wenye tabia hiyo kuacha mara moja.
Kuhusu watu wanaofoji viambatanisho vinavyomwezesha kupata passport, Msele amesema tatizo hilo limekuwa likisababisha usumbufu kutokana na baadhi ya wananchi kuleta viambatanisho bandia vinavyongiliana kimamlaka hasa kwenye vyeti vya kuzaliwa.