Thursday , 29th Sep , 2022

Mbaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini ambaye alipanga kufanya mauaji makubwa ya watu weusi nchini humo ikiwemo pia kufanya mapinduzi ya serikali amehukumiwa kifungo cha maisha jela.  

Bw.Harry Knoesen ( 64) alikua ni kiongozi wa kikundi cha kigaidi ambaye alipanga kuipindua serikali mnamo tarehe   28 Novemba 2019 , akitumia silaha nzito kama AK-47 , mabomu ya kurushwa kwa mkono na silaha nyinginezo. 

Mahakama kuu ya Mpumalanga  nchini humo imeelezwa kwamba Knoesen pia alipanga kutumia silaha za kibaiolojia ili kuwaua watu weusi .

Kwa mujibu msemaji wa wa mamlaka ya mwendesha mashata wa taifa  Bi.Monica Nyuswa,ilidaiwa  kwamba alitaka kufanya mambo hayo kwa kuwa aliagizwa na Mungu kuirejesha Afrika Kusini kwenye mikono ya watu weupe.