
Baadhi ya wananchi walioshiriki mazishi ya mtoto Aisha
Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi mkoani Kagera William Mwampaghale, amesema kuwa mtuhumiwa wa kwanza alikamatwa siku ya tukio na kumtaja mtuhumiwa mwingine ambaye alishirikiana naye kufanya mauaji hayo, ambaye pia amekamatwa na jeshi hilo Oktoba 03 mwaka huu
Kufuatia tukio hilo Mkuu wa mkoa wa Kagera Albert Chalamila, alikwenda kuhani msiba katika familia iliyopoteza mtoto huyo, na akiwa katika eneo hilo alisema kuwa jitihada mbalimbali zinafanyika kukomesha vitendo vya mauaji, na kwamba ndiyo maana vinafanyika vikao na watendaji wa vijiji, mitaa, kata na maafisa tarafa, ili kuhakikisha amani ya mkoa inakuwepo.
Siku ya tukio mtoto Aisha alitoweka nyumbani kwao na baadae baada ya msako kuanza mwili wake ulikutwa katika nyumba ambayo haijaisha iliyoko katika mtaa wa Matopeni.