
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt Jim Yonazi
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt Jim Yonazi, ametoa kauli hiyo leo Oktoba 7, 2022, jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano uliowashirikisha, wabunifu kwenye sekta ya TEHAMA uliolenga kuona namna bora ya kuzisaidia kampuni hizo za ubunifu kuweza kufanya biashara.
Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi wa huduma za kidigitali kutoka kampuni ya simu za mkononi nchini ya Vodacom Nguvu Kama do amesema Vodacom imeanzisha programu maalum inayofahamika kama Vodacom digital accelerator ambayo imelenga kuwasaidia vijana walioonyesha dhamira ya ubunifu kwenye uchumi wa kidigitali
Kwa upande wake mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu huria Cha Dar es Salaam Dkt. Cosmas Mnyanyi, ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya elimu maalum, ameshauri sekta ya TEHAMA isiwaache nyuma watu wenye mahitaji maalum.