
kikosi cha Singida Big Stars
Taarifa ya kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu iliyotoka leo Oktoba 7, 2022 imeeleza timu hizo zimefungiwa kutokana na kufanya usajili wa wachezaji hao ilihali wakiwa na mikataba na klabu zao za awali.
Taarifa hiyo imeeleza, Singida ilimsajili Metacha huku akiwa bado na mkataba na Polisi Tanzania hivyo hivyo kwa Prisons iloyomsajili Mbisa huku akiwa bado na mkataba na Coastal Union.
Kwa mujibu wa kamati hiyo, uamuzi huo umezingatia kanuni ya 47 (21) ya Ligi Kuu na hata hivyo, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imezikumbusha klabu zote nchini kuwa ussjili wa wachezaji unafanywa kwa kuzingatia kanuni na timu ambazo zitakiuka kanuni hizo, zitachukuliwa hatua.