
Yanga ilimvunjia mkataba kocha huyo Julai 27, 2020 baada ya kutoa maneno ya kibaguzi kwa mashabiki wa klabu hiyo.
Taarifa ya FIFA ilieleza Yanga imepewa siku 45 kuzilipa fedha hizo na wasipofanya ndani ya muda huo watafungiwa kusajili kwenye madirisha matatu.
Awali Yanga wao walipokuwa wanaachana na kocha huyo walitoa taarifa ikieleza ; ”Klabu ya Yanga inawaomba radhi viongozi wa nchi, Shirikisho la Soka Tanzania, wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yanga kutokana na kauli za kuudhi na kudhalilisha zilizotolewa na Eymael”.
Kocha huyo wakati anatimuliwa aliiacha Yanga ikiwa nafasi ya pili na kuifanya ishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.