Monday , 10th Oct , 2022

Shirika la umeme  nchini TANESCO Kanda ya Magharibi ikiwemo  Mkoa wa Tabora limewaonya watendaji kazi wake ambao wamekuwa na uzembe unaoambatana na mlolongo mrefu unaochelewesha huduma kwa wananchi.

Meneja wa TANESCO Kanda ya Magharibi Mhandisi Richard  Swai  wakati akizungumza na watumishi wa shirika hilo katika Mkoa wa Tabora amesema miongoni mwa malengo muhimu ya shirika  hilo  ni pamoja na kufikisha huduma maridhawa kwa wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa TANESCO  Mkoa wa Tabora  Mhandisi Hadija Mbaruku amesema pamoja na mipango  mingi katika uwajibikaji waliyonayo wamejipanga kuhakikisha wananchi wanafikishiwa huduma kwa wakati  bila vikwazo .