Wednesday , 12th Oct , 2022

Kutokana na kukithiri kwa matukio ya wizi kwa njia ya mtandao,Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini imesema haitosita kubadili kanuni na sheria katika kukabiliana na matukio hayo na kuwahakikishia usalama watumiaji wa mtandao.

Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo  cha masuala ya usalama mtandaoni kutoka Wizara ya Mawasiliano Steven Wangwe

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa utoaji elimu ya masuala ya usalama mtandaoni katika shule ya sekondari Jangwani Mkurugenzi Msaidizi wa kitengo  cha masuala ya usalama mtandaoni kutoka Wizara ya Mawasiliano Steven Wangwe amesema bado watanzania wengi hasa vijana wanakabiliwa na changamoto ya matumizi yasiyofaa ya mitandao na kuahidi kuendelea kutoa elimu kwao.

Kwa upande wake mwakilishi wa shule ya Sekondari Jangwani Mwalimu Philip Kilipamwambu amesema kwa sasa hakuna somo la elimu ya masuala ya usalama mitandaoni licha ya wanafunzi wengi kuendelea kujifunza matumizi ya vifaa vya TEHAMA.

Nao wanafunzi  wa Shule ya Sekondari Jangwani wanabainisha kuwa  bado wanafunzi wengi wanakosa elimu ya masuala ya usalama mtandaoni licha ya idadi kubwa ya vijana kujihusisha kazi mitandao kitu ambacho kina hatarisha maadili ya vijana wengi.

Hayo yanajiri katika maadhimisho ya mwezi wa elimu ya masuala ya usalama mitandaoni.