
Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 31 anaripotiwa kumshambulia mtoto wake kwa kutumia kitambaa cha plastiki sababu zinazotajwa kuwa ni kichanga hicho kuleta usumbufu wakati mwanaume huyo amelala .
Mke wa mwanaume huyo ameviambia vyombo vya habari kwamba mumewe alichukua simu yake na kumfungia yeye na mtoto katika chumba kimoja na kumtishia kutowaambia majirani. Hatimaye alitoroka siku mbili baadaye na kumpeleka mtoto wake hospitalini ambako madaktari walimkata mkono.
Dkt Chiedozie Mbalewe ambaye alimtibu mtoto huyo ameviambia vyombo vya habari kwamba kukatwa viungo hivyo kulifanyika ili kuokoa maisha ya mtoto huyo. Mtuhumiwa amekimbia na mama huyo ameripoti kesi hiyo polisi. Kundi la waandishi wa habari wanawake na tume ya kitaifa ya haki za binadamu wametaka haki itendeke.