
Jeneza lililobeba mwili wa mwanafunzi huyo
Baba wa marehemu Charles Lugwesa, amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11:00 jioni baada ya binti huyo kudai anasumbuliwa na tumbo hali ambayo iliwapelekea wazazi wote wawili kumchukua na kumpeleka zahanati ambako alipewa matibabu kwa muda mfupi na kufariki.
Taarifa zimeeleza kwamba, awali kabla mauti hayajamfika, mwanafunzi huyo alimwambia daktari kwamba amekunywa sumu ya panya na alipoulizwa sababu za kufanya hivyo hakujibu chochote.
Kwa upande wake viongozi wa dini na serikali ya kijiji cha Nyakahongola, wamewataka wazazi kutokuwa wakali kwa watoto wao wanapopata changamoto ili kuepusha kujichukulia maamuzi magumu.