
Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongella
RC Mongella ametoa agizo hilo wakati alipotembea moja ya mradi wa maji katika Kijiji cha Mfulonyi wilayani Arumeru unaotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), ambapo amebainisha kuwa mradi huo una mapungufu hivyo hautakuwa na tija kwa wananchi.
Nae Meneja wa RUWASA katika wilaya ya Arumeru Mhandisi Shabiri Waziri, ameeleza changamoto inayosababisha mradi huo kuchelewa kukamilika huku baadhi ya wakazi wakiomba kupewa kipaumbele katika suala la maji.