Thursday , 27th Oct , 2022

Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limefanikiwa kumuua mtu mmoja ambaye hajafahamika jina lake mwenye umri kati ya miaka 30 na 35  aliyekuwa anajihusisha na matukio ya unyanganyi wa kutumia silaha ambapo Oktoba 26 majira ya saa mbili usiku alifanya jaribio la kupora pikipiki

Kamanda wa Jeshi la Polisi  mkoa wa Kilimanjaro Simon Maigwa amesema jambazi huyo alikamatwa na pisto  aina ya Broin yenye namba A 920 580 ikiwa na risasi 9 

Kamanda Maigwa amesema uchunguzi wa awali umebaini silaha hiyo inamilikiwa na mtu ambae jina limehifadhiwa na iliibiwa kwa mmiliki huyo  ambae ni mkazi wa Manyara

 Jambazi huyo alikamatwa pia na silaha aina ya Sime ambapo mtuhumiwa alifariki wakati akipelekwa Hospitalini na mwili wake umehifadhiwa katika hiospital ya kanda ya KCMC Moshi